(Verse I )
Mimi Sayniza Yah Mugisa,
Nimejawa na shangwe kubwa siku ya leo.
Nina furaha kuwashukuru wazazi wangu
moyoni,
Kwa kunipa maisha mazuri kama haya.
Mulinifundisha kumhusu Yehova,
Na kuyapa maisha yangu kusudi.
Asanteni sana baba na mama wangu
(Chorus )
Nii pendeleo kubwa sana,
Kuwa Shahidi wa Yehova,
Katika ulimwengu huu mbovu.
Asante Yehova,
Kwa kutufundisha kukuhusu.
Mimi Sayniza nimejaa shangwe,
Na shukrani kwa kazi zako za ajabu.
(Verse 2)
Sitasahau kukushukuru,
Rafiki yangu mpendwa Shadrack Ben.
Tangu ulipoingia maishani mwangu,
Umekuwa nami, baraka ya kweli.
Mungu akupe maisha marefu
na mazuri.
(Chorus)
Ni pendeleo kubwa sana,
Kuwa Shahidi wa Yehova,
Katika ulimwengu huu mbovu.
Asante Yehova,
Kwa kutufundisha kukuhusu.
Mimi Sayniza nimejaa shangwe,
Na shukrani kwa kazi zako za ajabu.
(Bridge)
Ninashukuru sana kuwa na familia bora.
Ndugu yangu Filos Daniel,
Nafurahia sana bidi yako,
Yehova akubarīki sana.
Samsoni ndugu yangu,
Nafurahia ujasiri wako,
Kujikaza kwako hunipa furaha.
Yehova akupe maisha marefu.
Faraja wangu, nakupenda sana,
Yehova akuta jirishe kwa kumtumikia.
Dada yangu mdogo mpendwa,
Mrembo sana,
Shangwe,
Unanipa furaha kila wakati,
Yehova akufanikishe maishani mwako,
Akupe maisha marefu.
(Chorus )
Ni pendeleo kubwa sana,
kuwa Shahidi wa Yehova,
Katika ulimwengu huu mbovu.
Asante Yehova Baba,
Kwa kutufundisha kukuhusu,
Kwa kunipa tumaini na mwanga,
Wa kuiongoza njia yangu.
Mimi Sayniza nimejaa shangwe
Moyo wangu umejaa shukrani,
Kwa kazi zako za ajabu,
Wewe ni Mungu wa kweli.
Asante sana, asante sana,
Asante Yehova, Mungu wangu.
(Outro)
Wazazi wangu wapendwa
Yehova awape maisha marefu na mazuri.